Waziri wa Ardhi Angelina Mabula
Waziri wa Ardhi Angelina Mabula, amesema wamebaini kuwepo kwa vituo vingi vya mafuta ambavyo vimejengwa ndani ya hifadhi ya barabara huku wamiliki wa vituo hivyo wakiviendeleza na wengine wakiendelea kuvijenga licha ya zuio la serikali la hivi karibuni la kusitisha utoaji wa vibali vya ujenzi wa vituo hivyo.
Kuhusu migogoro ya ardhi hapa nchini Waziri ameeleza kupungua na iliyopo kwa sasa ni Ile ya kuanzia miaka ya 1985 mpaka 1990 lakini baada ya mwaka 2015 wanatatua ile ya zamani na kutoruhusu migogoro mipya ya ardhi
Aidha amesema wale ambao wamepewa ardhi na serikali na kutoiendeleza bado wanaendelea kuchukua hatua ikiwemo kunyang'anywa.