Virusi vya Corona
Taasisi hiyo ya KEMRI imesema kuwa hatua zilizochukuliwa mwezi Juni huenda zikasaidia kupunguza kusambaa kwa maambukizi hayo na kwamba maeneo yatakayoathirika na wimbi la nne ni Magharibi mwa Kenya, maeneo ya Ziwa Victoria, Nairobi na Mombasa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu katika Wizara ya Afya nchini Kenya Dkt. Patrick Amoth, amesema kuwa hatua zaidi zinahitajika kuchukuliwa ili kuepusha athari kubwa.
Hadi kufikia sasa jumla ya Kaunti 13 za Magharibi na Bonde la Ufa zimewekewa masharti ya kudhibiti maambukizi ya Corona, ikiwemo kutotoka ndani kuanzia saa 1:00 jioni na kuepusha misongamano kwa namna yoyote ile na hata maeneo ya ibada yamefungwa kwa siku 30.



