Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madhara ya zoezi la uzimaji simu feki sasa dhahiri

Ijumaa , 3rd Jun , 2016

Madhara ya zoezi la uzimaji wa simu bandia litakalofanywa na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA ifikapo Juni 16 mwaka huu yameanza kuonekana kwa wafanyabiashara wa simu eneo la Kariakoo ambao baadhi yao wamefilisika na kuanza kufunga biashara zao.

Wakizungumza na EATV iliyotembelea eneo hilo hii leo, wafanyabiashara hao wamesema kadri siku zinavyozidi kwenda wateja wamekuwa wakipungua kwa kasi huku wengi wakiacha kununua simu hadi lipite zoezi hilo wakiamini kwamba simu zitakazokwepo baada ya muda huo ndio zitakuwa simu halisi.

"Hili zoezi kwa kweli limesababisha baadhi yetu tufilisike kabisa...kama mimi hapa sina cha kuuza nimekula mtaji baada ya wateja kutofika dukani kwangu na sasa sina cha kuuza nimeamua kufunga duka nijaribu kufanya kitu kingine," amesema mmoja wa wafanyabiashara hao.

Wakiwa na nyuso zilizokata tamaa, wafanyabiashara hao wamesema kinachowaumiza sana ni mikopo waliyokopa kutoka taasisi za fedha ambayo wanatakiwa kuilipa kwa mujibu wa makubaliano waliyoingia na mabenki na taasisi husika za kifedha.

Aidha, katika kile walichokieleza kuwa ni madhara ya kisaikolojia; wafanyabiashara hao wameitaka TCRA kutobadilisha tarehe ya utekelezwaji wa zoezi hilo ili kurejesha imani kwa wateja kwani licha ya biashara ya simu, uchangamfu wa biashara katika eneo zima la Kariakoo hivi sasa umepungua.

"Kwa jinsi hali ilivyo sasa tunatamani hilo zoezi la kusima simu bandia litekelezwe haraka sana kwani tumekuwa tukiathirika kisaikolojia kwani kwa upande mmoja unaambiwa simu unazouza ni feki wakati sio kweli lakini wakati huo huo hata hizo simu halisi unazouza wateja wanaogopa kununua...sasa ni bora mbivu na mbichi zijulikane mapema," amesema mfanyabiashara Andrew Mashauri.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya