Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makalla agomea ujenzi wa Zahanati

Ijumaa , 29th Apr , 2016

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amegomea ujenzi wa Zahanati katika eneo la Ushirika kata Mpuguso wilayani Mbeya, kutokana na eneo hilo Kuwa katika mgogoro wa kimahakama.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla

Badala yake Makalla ameuagiza uongozi wa Kijiji hicho,kata na Wilaya kutafuta eneo jingine kwaajili ya kujenga zahanati hiyo itakayowezesha wakazi wa kijiji hicho na maeneo ya jirani kupata huduma za afya jirani.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa tamko la kupinga ujenzi wa Zahanati kwenye eneo la jirani na lilipo ghala na ofisi za kata ya Mpuguso alipozungumza na wakazi wa kijiji cha Kiwira jana kwenye mkutano wa hadhara ulioonekana kubeba hisia za watu wengi.

Makalla amekubaliana na baadhi ya wakazi wa kata hiyo waliosema mvutano uliozuka baina yao juu ya wapi zahanati ijengwe inatokana tu na tofauti za kisiasa ambapo baadhi ya wanasiasa wanataka kuutumia mgogoro huo kujinufaisha kisiasa.

Awali baadhi ya wakazi walisema kumekuwa na mgongano na mabishano baina yao kutokana na kile kilichoelezwa kuwa zipo tofauti za kisiasa baina ya uongozi wa kijiji cha Kiwira na ule wa kata ya Mapogoro.

Wamesema wakati mwenyekiti wa kijiji hicho anatokana na Chama cha Chadema,Diwani wa kata anatokana na Chama Cha Mapinduzi(CCM) hivyo kila upande umekuwa ukipendekeza sehemu yake ili kujenga Zahanati ya kijiji.

Hata hivyo baadhi ya wakazi wamesema wanachohitaji wao ni kujengwa kwa zahanati ili kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu kwenda katika hospitali teule ya Makandana ambako wamekuwa wakilazimika kutumia gharama kubwa za usafiri hususani nyakati za usiku wanapopeleka wagonjwa.

Kutokana na hali hiyo,mkuu wa mkoa amesema hayuko tayari kuona tofauti za kisiasa baina ya uongozi wa kata na kijiji zikiendelea kukwamisha maendeleo ya wananchi hivyo pande hizo zinapaswa kushirikiana na uongozi wa wilaya kutatua changamoto iliyopo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali