Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makonda aagiza kufunga maduka kumuenzi Nyerere

Jumapili , 13th Oct , 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema kuwa siku ya kesho maduka yote katika jiji la Dar es salaam yatafunguliwa kuanzia saa 5 asubuhi ili kupisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la mpifa kura kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na kuenzi miaka 20 ya kifo cha

Mwalimu Julius Nyerere.

Mhe. Paul Makonda ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumzia juu ya zoezi la uandikishaji wa wananchi kuelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na kuenzi kifo cha Baba wa Taifa.

Makonda amesema, "kesho Okt 14 ni kumbukizi ya miaka 20 tangu Baba wa Taifa atangulie mbele za haki, kwakuwa kesho ni siku ya mwisho ya kujiandikisha katika daftari la mpiga kura kuwapata Viongozi wa Serikali za Mitaa, kama Mkuu wa Mkoa wa DSM kwa kukuza demokrasia ndani ya Mkoa wetu naelekeza maduka yote yafunguliwe kuanzia saa 5 asubuhi hapa DSM kwakuwa hii ni sehemu ya kumuenzi Baba wa Taifa", amesema Makonda.

"Hii ni katika kuhakikisha wote tunajiandikisha ili kupata haki ya kupiga kura maana Baba wa Taifa aliwapa nafasi kubwa Viongozi hawa", ameongeza.

Kesho Oktoba 14, 2019 ni kumbukumbu ya kifo cha miaka 20 cha Mwalimu Julius Nyerere ambaye alifariki dunia Oktoba 14, 1994 akiwa katika matibabu nchini Uingereza. Pia kesho ni mwisho wa kujiandikisha kwa wananchi kwenye daftari la mpiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali