Mama Margaret Sitta akilia bungeni, kulia ni Marehemu Samwel Sitta.
Hayo yamejiri leo Januari 28, 2020, katika Mkutano wa 18 Kikao cha Kwanza, ambapo amesema kuwa jambo la kuwaenzi viongozi waliowahi kuongoza kiti cha Uspika ni jambo jema na la kihistoria.
"Joho hili daima litaendelea kuwa ni kumbusho la misingi ambayo aliisimamia marehemu, ikiwemo ukweli na uadilifu, kwa niaba ya familia tunawashukuru sana kwa tukio hili la heshima na la kihistoria" amesema Mama Sitta.
Viongozi wengine waliopokea majoho yao ni pamoja na Spika Mstaafu, Pius Msekwa na Mama Anne Makinda.