Jumatatu , 12th Oct , 2020

Serikali ya Mtaa wa Mwembeni Kata ya Manzese imesema kuwa inakabiliwa na changamoto ya uzoaji taka kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kushindwa kulipia tozo ya taka.

Mfano wa magunia yenye takataka

Akizungumza na Kurasa hii leo Mjumbe wa mtaa huo, Abdallah Juma, amesema kumekuwepo na mgogoro wa uzoaji taka baina ya wafanyabiashara waliopo eneo hilo wakidai kuwa fedha wanayolipia kwa ajili kitambulisho cha mjasiriamali kinajumuisha tozo hiyo.

Amesema adha hiyo imesabisha kutoelewana kati yao na wakandarasi sababu ya kushindwa kuwalipa fedha kwa ajili ya kuleta magari ya kubebea taka hizo

Naye Mwenyekiti wa mtaa huo, Nestory Kobelo, amesema kuwa inawalazimu kuondoa taka hizo wenyewe pindi zinapotolewa ili kuepusha uchafuzi wa mazingira.