Jumatano , 27th Jan , 2016

Serikali imesema kuwa mawaziri wakuu wastaafu wanahaki ya kuendelea kuhudumiwa na serikali kwa mujibu wa hitimisho la kazi namba 3 ya mwaka 1999 na kuendelea kupewa stahiki zao kwa mujibu wa sheria ya nchi inavyoelekeza.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe. Anjela Kairuki

Waziri wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe. Anjela Kairuki ameyasema hayo leo mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Dimani mhe. Hafidhi Ali Tahir ambaye alitaka ufafanuzi mawaziri wakuu wastaafu kujihusisha na siasa wakati huo huo bado wanahudumiwa na serikali na kuitaka sheria hiyo ifanyiwe marekebisho.

Waziri Kairuki amesema kuwa mawaziri wakuu wastafu wana haki ya kujiunga na chama chochote au kujihusisha na masuala ya kisiasa kwakua ni haki yao kikatiba na haki hizo haziwezi kuingiliwa.

Wakati huo huo Waziri Kairuki amekemea tabia ya watumishi wa serikali ambao wanahudumia jamii kwa kubagua matabaka ya vyama, kuwataka waache mara moja na watekeleze sera za serikali kwa kutambua kuwa nchi ina mfumo wa vyama vingi.