Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mch. Msigwa,afikishwa mahakamani mkoani Iringa

Alhamisi , 8th Oct , 2015

Mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia (CHADEMA), Mch. Peter Msigwa na wafuasi wengine watatu wa chama hicho wamefikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka yanayohusiana na uvunjifu wa amani pamoja na kuwashambulia askari wa jeshi la polisi.

Mgombea Ubunge jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kutoka Mahakamani Jana

Mchungaji Msigwa na wenzake watatu wamefikishwa mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa David Ngunyale na kusomewa mashitaka manne yakufunga barabara na kusababisha uvunjifu wa amani,kuharibu gari ya jeshi la polisi pamoja na kuwashambulia na kuwajeruhi askari polisi wawili akiwemo kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoani iringa.

Washitakiwa hao wanne ni sehemu tu ya watuhumiwa kumi wanaotuhumiwa kwa vurugu hizo zilizotokea siku ya tarehe 28 mwezi septemba, ambapo awali taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi iliwatuhumu wafuasi wa chadema kwa kufunga barabara na kuwafanyia vurugu wafuasi wa Chama cha Mapinduzi waliokuwa wametokea kwenye mkutano wa mgombea urais kupitia chama chao uliofanyika kwenye uwanja wa Samora

Washitakiwa wote wameachiwa kwa dhamana mpaka kesi yao itakapotajwa tena Novemba 2 mwaka huu ambapo mgombea ubunge wa jimbo la iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amesema pamoja na mashitaka hayo wanachadema hawapaswi kukata tamaa ya kufanya kampeni za amani ili kuhakikisha wanashinda.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa