Jumatano , 16th Dec , 2015

Halmshauri ya wilaya ya Hai imeamuru kukamatwa kwa meneja wa mamlaka ya maji ya wa wilaya hiyo Rojas Marando pamoja na mhasibu wa mamlaka hiyo Devotha Mwambuli kwa tuhuma za kufanya ubadhirifu wa shilingi milioni 98 kwa ajili ya mita za maji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw, Said Mderu

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw, Said Mderu amesema hatua hiyo inafuatia kikao cha pamoja cha kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ambapo wamebainika kufanyika kwa ubadhirifu huo mwezi Oktoba mwaka 2015.

Mkurugenzi huyo amesema meneja huyo na muhasibu wake wamebainika kufanya ubadhirifu huo kwa kuagiza mita za maji zenye gharama za sh. milioni 98 kutoka Ujerumani ambapo walifanya hivyo huku kwa kukiuka sheria ya manunuzi.

Kwa upande wako mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka na mbunge wa wilaya hiyo Mh. Freeman Mbowe wamesema kuwa mamlaka hiyo kwa kuwa ilikuwa inafanya kazi kama chombo kinachojitegemea kiasi cha kuleta mgogoro katika uendeshaji wake.