Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mhagama,wanawake viongozi wakemea vurugu uchaguzi

Jumamosi , 24th Oct , 2020

Ikiwa zimebaki siku tatu kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Tanzania,wanawake viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa wamekemea vikali vitendo vya uvunjifu wa amani kwa wale wote wenye nia ovu ya kutaka kuvuruga Uchaguzi huo.

Waziri wa Nchi, Sera,Bunge,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu,Jenista Mhagama

Wakizungumza hii leo katika mkutano na waandishi wa habari,kupitia Katibu Mtendaji Anna Ryoba Paul, wanawake viongozi  wamelipongeza jeshi la polisi kwa jitihada zake za kulinda amani katika kipindi hiki cha uchaguzi.

'' Pia tunawataka viongozi wa siasa kutotumia viongozi wa dini katika siasa ili kuepusha mgawanyiko miongoni mwa wananchi ''Alisema katibu huyo Anna Paul

Naye Waziri wa Nchi, Sera,Bunge,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu,Jenista Mhagama, ameungana na viongozi hao kwa kuzungumza nao kwa njia ya simu katika mkutano huo na kusema kuwa hatua hiyo ni nzuri  kwa nafasi walionayo na ni jukumu lao kulinda na kudumisha amani ya nchi yao.

''Kukutana kwenu kuna umuhimu katika kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi mnaowataka na mna jukumu kubwa la kuhamasisha na kuilinda amani ya nchi.''Mh. Jenista aliongeza

Aidha Mh. Jenista amesema kuwa waathirika wakubwa iwapo amani na utulivu vitatoweka ni wanawake  na  kuwaasa watu wote kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi hivyo ni muhimu kuilinda amani ya nchi na siku ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa