Meya wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto
Akizungumzia hilo kwenye show ya DADAZ ya East Africa TV Mhe. Omary Kumbilamoto amesema kesho watakuwa na kikao na wajane wa Vingunguti kujadili na kutengeneza mazingira ya kuelekea siku ya wajane duniani.
"Mimi kule vingunguti kama Mume wao, namiliki wajane takribani 290, hawa ni kina mama ambao wamefiwa na waume zao kwa hiyo lazima tuwaliwaze ndio maana nipo nao karibu, tuna kikao kesho cha kuzungumzia ni namna gani tutangeneza mazingira kuadhimisha siku ya wajane duniani" amesema Omary Kumbilamoto





