Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miss wa gereza ahukumiwa Kifo

Alhamisi , 19th Jul , 2018

Mlimbwende wa taji la urembo katika gereza kuu la wanawake la Lang'ata (Miss Lang’ata Prison 2016)  Jijini Nairobi amehukumiwa kifo baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake aliyefamika kwa jina la Farid Mohamed mwaka 2015.

Bi. Ruth Wanjiku Kamande (Miss Lang’ata Prison 2016.

Mrembo huyo mwenye jina la Ruth Wanjiku Kamande amepatikana na kosa la kumuua mpenzi wake huyo katika mtaa wa Buruburu, Nairobi mnamo tarehe 20 Septemba, 2015 baada ya kuwa na mvutano kati yao.

Jaji Jessie Lessit amesema upande wa mashtaka ulithibitisha kumkuta mshatikiwa na hatia pasipo kuwa na shaka yoyote ambapo amedai kwamba  vitendo vya Kamande vilionyesha aliua kwa kukusudia.  

Kwa mujibu wa vyombo vya habari kutoka Kenya vimeripoti kwamba mrembo huyo alijitetea kwamba mzozo kati yake na mpenzi wake ulikuja pale alipoiona kadi ya hospitali iliyoashiria kwamba Mohammed alikuwa akipokea matibabu ya Ukimwi. 

Aidha ameeleza kwamba mpenzi wake huyo (marehemu Mohamed) alimwambia wakati huo ni heri wafe wote kuliko hali yake ya Ukimwi ifahamike hadharani ambapo wakati mzozo ukiendelea ulimpelekea kumchoma na kisu kilichokuwa kinachotumiwa jikoni. 

Pamoja na hayo mahakama imekataa utetezi wa Bi Wanjiku wa kwamba marehemu alijaribu kumbaka ambapo ilielezwa kuwa uchunguzi wa madaktari ulionyesha hakukuwa na ukweli kuhusu madai hayo.

Wanjiku kwa sasa ambaye ana umri wa miaka 25 wakati anakamatwa ndiyo alikuwa amejiunga na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kusomea masuala ya biashara, kwa mujibu wa wakili wake.

Wanjiku amekuwa mahabusu tangu mwaka 2015 katika gereza la Lang'ata  akisubiri maamuzi ya mahakama dhidi ya shtaka lake.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali