Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkapa apumzishwa rasmi kijijini Lupaso

Jumatano , 29th Jul , 2020

Safari ya Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, imefika tamati rasmi hii leo baada ya kupumzishwa katika nyumba yake ya milele kijijini Lupaso, Wilayani Masasi Mkoani Mtwara. 

Marais Wastaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete,na Ali Hassan Mwinyi, pamoja na Rais John Pombe Magufuli, wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais Mstaafu Marehemu Benjamin Mkapa.

Mkapa amezikwa kwa kuzingatia taratibu za imani yake ya Kikatoliki pamoja na taratibu za kiserikali ambapo amepigiwa mizinga ya kijeshi 21, ikiwa ni sehemu ya heshima kwa kiongozi huyo wa zamani.

Shughuli  ya mazishi ya kuhitimisha safari yake imefanyika katika viunga vya nyumbani kwao Lupaso, ambapo mamia ya wananchi miongoni mwao wakiwa ni viongozi waandamizi wa Serikali, wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania pamoja na Marais wastaafu.

Mzee Mkapa anapumzishwa ikiwa imesalia siku moja tu, kati ya zile saba za maombolezo zilizotangwazwa na Rais John Magufuli, alipokuwa akitangaza kifo cha Hayati Benjamin Mkapa, usiku wa kuamkia Julai 24. 

Aidha Mzee Mkapa, anatajwa kuwa Rais wa aina yake kutokana na mageuzi ya kimfumo aliyoyafanya enzi za utawala wake (1995 -2005), ambapo pamoja na mambo mengine alianzisha taasisi mbalimbali za umma, ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA). 

Zaidi Mzee Mkapa katika upande wa Kimataifa anakumbukwa kama msuluhishi na mwanadiplomasia mahiri, aliyejitolea kuleta amani katika mataifa mbalimbali, ikiwemo Burundi.

Pumzika kwa Amani Rais wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali