Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkapa asikitishwa na mkataba wa EPA

Alhamisi , 9th Apr , 2015

Rais mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania, Mhe. Benjamin William Mkapa, ameelezea kusikitishwa na jinsi Tanzania pamoja na nchi nyingine za Afrika Mashariki, zilivyosaini mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi na Jumuiya ya Ulaya.

Rais mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania, Mhe. Benjamin William Mkapa,

Rais mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania, Mhe. Benjamin William Mkapa, ameelezea kusikitishwa na jinsi Tanzania pamoja na nchi nyingine za Afrika Mashariki, zilivyosaini mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi, baina ya Jumuiya ya Ulaya na nchi za Afrika, Karibeani na Pasifiki, mkataba unaojulikana kwa kifupi kama EPA (Economic Partnership Agreement).

Akizungumza na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mkapa ameutaja mkataba huo kuwa ni aina nyingine ya ukoloni kama ilivyokuwa kwa mkataba wa Berlin wa mwaka 1880, ambapo nchi za Ulaya zililigawa bara la Afrika kwa ajili ya manufaa yao kiuchumi.

Amesema kupitia mkataba huo, ni vigumu kwa kampuni za kiafrika kushinda zabuni katika nchi za Ulaya lakini ni rahisi kwa kampuni za Ulaya kushinda zabuni katika nchi za Afrika kutokana na kukomaa kiteknolojia, na hata zinaposhindanishwa kampuni za Afrika na Ulaya ni rahisi kwa kampuni za Ulaya kushinda, jambo litakalochangia kuua kampuni za kiafrika

Mhe. Benjamin William Mkapa, amewataka watumishi wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa kuwa wazalendo linapokuja suala la kujadili masuala mbali mbali yanayohusu maslahi ya nchi.

Mkapa amesema dhana ya uzalendo ni muhimu kwa watumishi hao hasa nchi inaposaini makubaliano mbalimbali ya kimataifa.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe, amesema kusainiwa kwa mkataba huo ni matokeo ya kukosekana kwa ushirikiano baina ya wizara yake katika mikataba ya kimataifa, ambapo ameahidi kuonana na Spika wa Bunge Bi. Anne Makinda kwa lengo la kuwasihi wabunge wasiridhie mkataba huo alioutaja kuwa ni wa kinyonyaji.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa