Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkuu wa Shule atafuna ada, Serikali yamjia juu

Jumanne , 19th Jan , 2021

Serikali mkoani Geita imeuagiza uongozi wa shule ya sekondari ya Geita Islamic, ifikapo kesho asubuhi iwasilishe stakabadhi za malipo ya mitihani ya wanafunzi, baada ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo kukiri kula ada za mitihani ya Taifa ya wanafunzi wa kidato cha Pili na cha Nne.

Afisa Elimu wa mkoa wa Geita, Arnold Msuya

Akizungumza hii leo Januari 19, 2021, Afisa Elimu wa mkoa wa Geita, Arnold Msuya, amesema kuwa kitendo cha mwalimu huyo kula ada hizo, kimepelekea wanafunzi hao kukosa matokeo yao yaliyotangazwa hivi karibuni na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), ambapo kutokana na hali hiyo akaelekeza suala hilo lishughulikiwe na wanafunzi wapate matokeo yao.

"Tulipokea malalamiko kutoka kwa wazazi wa wanafunzi hao kwamba walilipa ada ya mitihani lakini matokeo ya watoto wao hayakutoka, nimemuelekeza mmiliki wa shule hiyo ifikapo kesho saa 4:00 asubuhi alete risiti za malipo ili matokeo yao yatoke, kama mkuu wa shule alipokea ada na akatoweka nazo hilo si jukumu la mzazi tena ni jukumu la mwenye shule aliyeruhusu fedha zikusanywe na kuwekwa mfukoni", amesema Arnold.

Kwa upande wake, Meneja wa shule hiyo Mussa Mnyita, amesema kuwa wazazi walikamilisha malipo hayo kutokana na changamoto ya mwalimu huyo kutolipa malipo hayo NECTA na kwamba uongozi wa shule utawajibika kulipa malipo hayo.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali