
Moto huo ambao uliozuka usiku wa kuamkia leo Jumatatu Agosti 22/2022 uliteketeza pia nyumba tano za wananchi wa eneo hilo
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo mpaka sasa hakijulikani
Amesema moto huo umesababisha hasara kubwa ya kuteketeza magari yaliyokuwa na shehena za mafuta, mizigo pamoja na nyumba zilizokuwa karibu na eneo hilo na kwamba thamani halisi ya mali zilizoteketea bado haijajulikana kutokana na udharura wa tukio hilo
Amesema hadi sasa hakuna mtu aliyepoteza maisha katika ajali hiyo licha ya kwamba mtu mmoja ambaye alikuwa anasaidia kuokoa mali kuungua kwenye unyayo
“Moto huo ulizuka majira ya saa tano usiku na kuteketeza magari matano na kuunguza mali na samani zilizokuwa kwenye nyumba tano zilizokuwa karibu na eneo hilo na tunamshukuru mungu madhara kwa binadamu sio makubwa,” ameeleza Mfune.
Ameongeza kuwa gari la zimamoto lilifika katika eneo la tukio saa 7:00 usiku lakini magari manne yalikuwa tayari yameshateketea na hivyo likatumika kuzima gari moja ambalo pia kwa sehemu lilikuwa limeteketea kwa sehemu kubwa.
Amedai kuwa chanzo cha moto kinahisiwa kuwa ni baadhi ya watu kujaribu kuiba mafuta kwenye magari yaliyokuwa yameegeshwa katika eneo hilo na kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo halisi cha moto huo.
Alitoa tahadhari kwa wananchi wa eneo hilo kuepuka kusogelea moto bila tahadhari kwa maelezo kuwa moto ni hatari na kwamba kuna uwezekano likatokea tatizo kama ilivyotokea Morogoro ambalo watu wengi walifariki