Orodha ya mawaziri na naibu mawaziri imepunguzwa kutoka 33 hadi 27, lakini wakosoaji wanasema bado ni kubwa mno.
Mabadiliko hayo yalitarajiwa kufuatia ripoti kwamba mawaziri kadhaa walihusishwa na uchunguzi wa ufisadi unaofanywa na Taasisi ya Kupambana na Rushwa ya Malawi (ACB) na Shirika la Uhalifu la Kitaifa la Uingereza.
Katika ujumbe wake wa mwaka mpya, Rais Chakwera alikuwa ameahidi kutaja baraza jipya la mawaziri. Orodha ya waziri mpya wa baraza la mawaziri ilitolewa Jumanne usiku wa manane saa za eneo Malawi.
Bw Chakwera hajajitengea cheo cha uwaziri kama ilivyokuwa hapo awali. Pia hakutenga majukumu ya uwaziri kwa makamu wake wa rais Saulos Chilima ambaye anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi ambayo anakanusha.
Makamu wa rais bado yuko madarakani kwa sababu chini ya sheria za Malawi hawezi kufutwa kazi.
Wanachama waandamizi wa chama hicho kutoka muungano tawala pia waliachwa nje ya baraza jipya la mawaziri.



