Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Msafara wa Mbowe wavamiwa na Morani

Ijumaa , 14th Sep , 2018

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe, umevamiwa na kundi la Morani wakimpokea na kumlaki wakati akiwasili wilayani Monduli mkoani Arusha kwa ajili ya kampeni za Chama chake zinazoendelea katika jimbo hilo leo.

Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe akipokelewa jijini Arusha.

Baada ya kulakiwa Mbowe ametoa hotuba yake kwa wakazi wa Monduli kuwa ifike mahali waachwe washindane kwa hoja na sio siasa za chuki kama ambavyo baadhi ya viongozi wanafanya katika mikutano ya kampeni kwani wote wamepewa mamlaka na wananchi ambao ndio wapiga kura.

Tusihukumiwe kwa tofauti zetu, tusihukumiwe kwa historia zetu, tulumbane kwa hoja”, amesema Mbowe.

Kwa upande wake mgombea wa Ubunge jimbo la Monduli (CHADEMA) Yohana Masiaya amesema kuwa hatolishusha hadhi jimbo la Monduli na kurejesha heshima ya jimbo hilo kulingana na historia yake ikiwemo kuongozwa na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa.

CHADEMA wanamnadi mgombea wao Yohana Masiaya ambaye anapigania kiti cha Ubunge kwa kupitia jimbo la Monduli ambalo awali lilikuwa likishikiliwa na Mbunge wa CHADEMA, Julius Kalanga kabla ya kujivua Ubunge na kukihama chama hicho kisha kukimbilia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Agosti 4, 2018, tume ya taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo matatu ya Monduli, Ukonga na Korogwe Vijijini na wa udiwani katika kata mbili za Tanzania Bara utakaofanyika Septemba 16, mwaka huu, ambapo kampeni zilianza Agosti 21 na zitamalizika kesho Jumamosi Septemba 15.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi