Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mtia nia wa Urais CHADEMA adai hana anayemhofia

Alhamisi , 18th Jun , 2020

Mtia nia wa kugombea nafasi ya Urais kupitia CHADEMA, Leonard Manyama, amesema kuwa miongoni mwa majina 11 ya watia nia yaliyotangazwa na chama hicho, haoni hata mmoja ambaye anaweza akamzidi na hivyo yeye ndiyo atapewa ridhaa ya kupepeperusha bendera ya chama.

Leonard Manyama, Mtia nia wa kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA.

Manyama ameyabainisha hayo leo Juni 18, 2020, wakati wa mazungumzo maalumu na EATV&EA Radio Digital, ambapo pia amevitaja vipaumbele vyake katika siku 100 za kwanza pale atakapokuwa amechaguliwa na wananchi, ikiwemo kujenga Taifa lenye umoja na mshikamano, kwa madai ya kuwa vitu hivyo havijafanyika tangu mfumo wa vyama vingi uanze hapa nchini.

Aidha amesisitiza kuwa ataliunganisha taifa katika masuala ya Mungu, uhuru wa vyombo vya habari na kwamba katika utawala wake hatoogopa kunyoshewa vidole kwa kuweka usawa kwa kila mtu

"Wagombea wote waliojitokeza kutangaza nia wana uwezo na sifa stahiki, mimi ninategemea kwa kila mmoja wetu anaweza kuchaguliwa na chama, na katika wote tuliochaguliwa sina ninayemhofia ila ninawaheshimu wanachama wenzangu" amesema Manyama.

CHADEMA tayari imekwishawatangaza watia nia 11 wa kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwemo Lazaro Nyalandu, Tundu Lissu, Freeman Mbowe, Peter Msigwa, Richard Simba, Shaban Msafiri na wengine.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali