Alhamisi , 3rd Feb , 2022

Ginasa Petro (30) aliyekuwa mkazi wa kijiji cha Kayenze, kata ya Kafita wilaya ya Nyang'hwale, amejiua kwa kunywa sumu ya Panya baada ya mke wake Sarah Jeremia kukataa kurudi kuishi naye baada ya hapo awali kuondoka kutokana na mgogoro wa kimapenzi.

Sumu

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba wivu mkubwa ndiyo uliopelekea mwanaume kuchukua maamuzi hayo na kusihi kwamba wanandoa wanapaswa kuwaona viongozi wao wa dini ili kusuluhisha changamoto zao na si kujitoa uhai.