
Mama huyo ameacha watoto wawili wadogo
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kipingu Alphonce Mbeya anasema tukio hilo limetokea Agosti 13 majira ya saa 12 jioni wakati mwanamke huyo akiwa na wenzake wakifata huduma ya maji kwa matumizi ya nyumbani ambapo inaelezwa hadi tukio hilo limetokea tayari watu 4 wameshambuliwa na mamba wakisaka maji
Mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ludewa wamelazimika kufika msibani kuwapa pole wafiwa na kisha kuahidi kutatua changamoto ya mradi wa maji katika kijiji hicho huku pia wakitoa agizo kwa wizara ya mali asili na utili kuwavuna mamba katika mto huo ili kunusuru vifo vinavyoweza kuzuilika.