Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwanri afafanua kauli yake "Mungu amshukuru Rais"

Jumatatu , 22nd Apr , 2019

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Agrey Mwanri amefafanua kauli yake ya kumtaka Mungu amshukuru Rais Magufuli ambayo aliitoa hivi karibuni ambapo amesema kauli hiyo ililenga kumshukuru kiongozi huyo kwa mambo anayoyafanya kwa sasa katika kuleta maendeleo.

Akizungumza na waandishi habari Mjini Tabora Mwanri amedai suala hilo, lilipata tafsiri potofu kwa baadhi ya watu hasa kupitia mitandao ya kijamii.

"Nilichokuwa nalenga pale ni hiki hapa mfano nitoe kwenu kwa waandishi wa habari mara nyingi mnatuunga mkono Serikali katika kuleta maendeleo ya Tabora, inafika mahali katika kuzungumza na waandishi wa habari nawaambia uwezo wa kushukuru sina, nitachofanya kumuomba mwenyezi Mungu awashukuru kwa kazi nzuri mnayofanya." amesema Mwanri

Mwanri ameongeza kuwa "mimi nimekuwa nikiwaambia hata wananchi kuwa mimi siwezi kuwashukuru bali nitamwachia Mungu awashukuru, ila nilichosema siku ile ni nilimaanisha Rais Magufuli anafanya kazi nzuri na ni mambo makubwa yaliyotufurahisha mioyo yetu, ninachoweza kusema na kufanya ni kumuomba Mungu atusaidie kumshukuru Rais Magufuli, japo jambo lile lilipata tafsiri potofu"

"Ila nilichojifunza inapopelekwa habari kama ile masikio yanayopokea ni mengi usifikiri hata kama uko sawa ukafikiri utapokea kwa hisia hivyohivyo, kama masikio mengi yalipokea jambo hilo kwa tofauti sina cha zaidi ya kuomba msamaha kwa sababu nimeshafafanua na mimi ambao walininukuu vibaya natangaza nimeshawasamehe, ni Mungu peke yake hakuna binadamu atakayeweza kuchukua nafasi ya Mungu, nitakuwa nimechuja sana nikiamini binadamu anaweza kuchukua nafasi ya Mungu" amesema Mwanri

Mwanzoni mwa mwezi Aprili Mkuu wa huyo wa Mkoa alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini juu ya kutoa kauli ambayo alieleza kuwa anamuomba Mungu amshukuru Rais Magufuli hali iliyomfanya kuzua taharuki kwenye mitandao ya kijamii.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa