
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Ruvuma, Jackline Msongozi
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na wananchi pamoja na wakulima wa mkoa wa Ruvuma.
"Wakati naingia madarakani wapo walionidharau kwamba sijasoma, lakini wakati naomba hiyo nafasi niliguswa moja kwa moja na shida za wanawake na wananchi wengine wadogo wadogo katika masuala ya kilimo, ndiyo maana nilisema nijitahidi nifanye kazi ili wale waliokuwa wanadharau waone nimefanya hata robo," amesema Mbunge Jackline.