Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwili wa Mama Mercy Anna Mengi waagwa

Alhamisi , 8th Nov , 2018

Askofu wa Kanisa la Kiinjili Kiluteri Tanzania (KKKT), Dayosisi na Mashariki na Pwani, Askofu Alex Malasusa amewataka watu waendelee kumuombea aliyekuwa moja ya waanzilishi wa makampuni ya IPP Mama Mercy Anna Mengi ambaye alifariki dunia Oktoba 31 mwaka huu.

Familia ya Mama Mercy Anna Mengi wakiwa kanisani Azania Front katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu.

Akizungumza katika ibada maalum ya kuuaga mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi ambao ilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa kitaifa ambapo Askofu Malasusa alinukuu neno la Biblia kutoka Paulo 4 mstari 13 hadi14 na Paulo 5 mstari 1 hadi 2.

Jambo kubwa na la maana kwetu sisi ni kuwa na uhakika kwa mungu kwa kushika na mapenzi yake, na hata katika hili tuyakubali mapenzi yake kama inavyosema sala yake, ili tuendelee kuishi kwa mapenzi yake,” amesema Dkt Alex Malasusa.

Askofu Malasusa amesema “Mungu ameweka siri kubwa kwenye suala la kifo, hata sisi wachungaji Mungu ametuficha bali ni siri yake yeye mwenyewe Mungu, niwaombe ndugu jamaa tuendelee kujiweka karibu nayeye ili kila mtu afikie tamanio la kwenda mbinguni.”

Miongoni mwa watu walioshiriki ibada hiyo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.

Ibada hiyo iliyofanyika Jijini Dar es salaam, ilianza majira ya saa 6 mchana na kuongozwa na Askofu wa kanisa hilo,  Dkt Alex Malasusa akisaidiwa na msaidizi wake Chadiel Luiza.

Mwili wa Mama Mercy Mengi unatarajiwa kusafirishwa kuelekea Machame Moshi kwaajili ya maziko Jumamosi Novemba 10, 2018.

Mama Mercy Anna Mengi atakumbukwa kama moja ya waanzilishi wa makampuni ya IPP ambayo inamiliki vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo EATV, EA Radio, ITV, NIPASHE, The Guardian, Radio One, na Capital Radio.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke