Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naibu Waziri alalamikia usalama jimboni kwake

Jumatatu , 24th Sep , 2018

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji na Mbunge wa Jimbo la Pangani Juma Aweso amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuongeza umakini wa hali ya ulinzi katika jimbo lake la Pangani kufuatia kifo cha dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Sharo.

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji na Mbunge wa Jimbo la Pangani Juma Aweso (kushoto) na marehemu Sharo aliyekuwa dereva wa bodaboda, (kulia).

Kupitia ukurasa wake wa kijamii Naibu Waziri Juma Aweso ameonesha kuguswa na kifo cha kijana huyo ambaye inatajwa alikua dereva wa bodaboda wilaya Pangani na  anadaiwa kunyongwa na watu wasiojulikana na kumuibia pikipiki.

Naibu Waziri Aweso ameandika “Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya kifo cha kijana mwenzangu maarufu kwa jina la Sharo kilichotokea kwa kunyongwa jimboni Pangani..,Nikiri kua jambo hili limenigusa na kuniumiza sana,nimepeleka hisia zangu mbali na kuwaza kijana asie na hatia anayehangaika kufanya kazi kutimiza malengo yake anakatizwa uhai wake kwa ajili ya wizi wa pikipiki na kupoteza maisha,ama kwa hakika inasononesha sana…”

Nitoe wito kwa serikali tena kwa hisia kali ikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama kuliangalia suala hili kama jambo la dharula na kulitafutia ufumbuzi wa kudumu kwani sio mara ya kwanza inatokea.” Aliongeza Naibu waziri Aweso

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari