Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Namthamini kuongeza ufaulu kwa wanafunzi

Jumatano , 31st Jul , 2019

Kampeni ya Namthamini ya East Africa Television na East Africa Radio, imeendelea kuhakikisha wasichana wote shuleni wanasoma vizuri wakiwa wanapata taulo za kike.

Leo Julai 31, 2019 timu ya Namthamini imefika wilayani Hanang katika shule ya Sekondari Simbay, iliyopo takribani Kilometa 30 kutoka mjini na kukabidhi Pedi kwaajili ya wasichana 114 ambazo watazitumia kwa mwaka mzima.

Akiongea wakati wa kupokea taulo hizo, Mkuu wa Wilaya ya Hanang Joseph Mkirikiti amesema Kampeni ya Namthamini ya East Africa Television imesaidia kuongeza ufaulu kwasababu inawasaidia wanafunzi kusoma bila kukosa masomo.

"Niwashukuru East Africa Television kupitia kampeni hii naamini ufaulu utaongezeka kwa wasichana maana mmetatua changamoto yao kubwa inayowafanya wakose masomo", amesema Mkirikiti.

Kwa upande wake Mwalimu wa taaluma Madam Christina, akiongea kwa niaba ya mkuu wa shule hiyo ameeleza kupokea kwa furaha msaada huo na kusema kuwa suala la hedhi huwa linachangia utoro kwa wanafunzi.

"Sasa naamini wanafunzi wangu watafaulu kwasababu nitawaona shuleni siku zote tutaondokana na ruhusa kwasababu ya hedhi ambazo zilikuwa zinawafanya mkose mtiririko wa vipindi", amesema.

Shule ya Simbay ni shule ya kutwa yenye jumla ya wanafunzi 207, Wavulana wakiwa ni 94 na wasichana 114.

 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa