Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nanyamba walia na tatizo la maji safi na salama

Jumatano , 16th Sep , 2015

Wakazi wa halmashauri ya mji wa Nanyamba mkoani Mtwara wamelalamikia tatizo la uhaba wa maji lililodumu kwa miaka mingi kiasi cha kulazimika kusafiri umbali wa kilomita zaidi ya 50 mpaka Ruvuma kufuata huduma hiyo.

Aliekua Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Amina Makilagi akipanda ngazi za tanki la maji la mradi wa Maji wa Nanyamba.

Wakizungumza na East Africa Radio, baadhi ya wananchi hao walisema maji wanayotumia sio salama kwasababu ni ya mabwawa ambapo hata hivyo upatikanaji wake wanalazimika kusafiri kwa zaidi ya kilomita 10, hali inayopelekea kuzorotesha shughuli zingine za kimaendeleo.

Aidha, mgombea ubunge wa jimbo la Nanyamba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdallah Chikota, ambaye amekosa mpinzani katika jimbo hilo ameahidi kutatua tatizo hilo, kwa kufufua na kuanzisha miradi mingine ya maji.

Kwa upande wake, mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Oscar Ng’itu, amesema zipo baadhi ya changamoto ambazo zinapelekea uwepo wa tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kukosa nishati ya uhakika katika vyanzo vya maji na kulazimika kutumia mafuta kiasi cha zaidi ya lita 150 kwa siku kwa ajili ya kuwasha jenereta, ambalo haliwezi kufanya kazi kwa saa 24.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil