Muonekano wa gari la Nape.
Nape amepata ajali hiyo wakati alipokuwa anaelekea wilayani Liwale kuungana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Taifa Dkt. Bashiru Ally anayezuru wilayani Liwale
Aidha, inadaiwa hakuna madhara makubwa yaliyotokea kwa waliokuwa ndani ya gari ambapo kwa sasa Mbunge Nape amepatiwa usafiri mwingine ili kusudi aweze kuendelea na safari yake ya kuelekea wilayani Liwale.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema wameanza kuchunguza chanzo cha ajali hiyo licha ya kuwa eneo lililotokea ajali hakuna hitilafu ya aina yoyote.