Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nassari kutimkia CCM, ofisi ya Mbunge yanena

Jumatano , 24th Oct , 2018

Baada ya kusambaa kwa taarifa zilizodai kuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kutimkia Chama cha Mapinduzi (CCM) na kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge na uanachama wa CHADEMA, ofisi ya mbunge huyo imekanusha taarifa hiyo.

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu wa ofisi ya Mbunge huyo leo Oktoba 24, Julius Ayo imesema kuwa, Nassari hayupo nchini na amekwenda nchini Marekani kwa shughuli za kikazi kuhusiana na jimbo lake.

"Habari zinazo sambaa mitandaoni tangu juzi kuhusu Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kujivua Ubunge na Kujiunga na CCM siyo za kweli, puuzeni habari zinazo sambazwa na wajinga wachache", amesema Julius.

Kupitia mitandao ya kijamii zilisambaa taarifa zilizodai kuwa Nassari amejiunga na CCM ili kuunga mkono jududi za Rais Magufuli na kujivua nafasi yake ya Ubunge kupitia CHADEMA.

Mpaka sasa jumla ya Wabunge tisa wa upinzani wamejiunga na CCM, ambao ni Maulid Mtulia (Kinondoni), Godwin Mollel (Siha), Julius Kalanga (Monduli), Mwita Waitara (Ukonga) ambapo wanne hao walipojiunga CCM walipitishwa kuwania ubunge na kuibuka na ushindi.

Wengine ni Zuberi Kuchauka (Liwale) ambaye pia ameshinda ubunge katika jimbo hilo kwenye uchaguzi uliokaofanyika Oktoba 13, 2018, huku ambao wanasubiri uchaguzi wa marudio kwa sasa ni aliyekuwa Mbunge wa Ukerewe (CHADEMA) Joseph Mkundi, Mbunge wa Babati (CHADEMA) Pauline Gekul, James Ole Millya (CHADEMA) Simanjiro na Marwa Chacha aliyekuwa mbunge wa Serengeti kwa tiketi ya CHADEMA.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali