Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Natakiwa kuombwa msamaha'' - Sugu

Jumatatu , 21st Mei , 2018

Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu amedai kwamba anatakiwa kuombwa msamaha kutokana na hukumu aliyopewa ya kutumikia kifungo jela bila sababu za msingi.

Sugu amesema hayo leo Mei 21, 2018 katika viwanja vya Bunge Jijini, Dodoma ikiwa ni kikao chake cha kwanza cha bunge kuhudhria tangu ameachiwa huru baada ya kuhudumu kwa siku 73 katika Gereza la Ruanda, Mbeya, ameongeza kwamba bila kujali ni nani amempa msamaha lakini anastahili kuombwa msamaha kwa hukumu aliyopewa.

“Mimi naamini sikutakiwa kuwa ndani, na unapozungumzia suala la msamaha nabaki najiuliza, napewaje msamaha na mtu ambaye amekufunga, mtu ambaye wanasema ulimfedhehesha, kitu cha msingi sio nani kanipa msamaha, mimi siamini kana nastahili kupewa msamaha bali natakiwa kuombwa msamaha kwa kufungwa kiholela na kutoka kiholela” amesema Sugu.

Mbunge huyo ameongeza kuwa wafungwa pamoja na askari katika Gereza la Ruanda walishangaa kumuona mbunge huyo katika Gereza hilo, Sugu amesema “wafungwa na askari walinipokea vizuri, kwanza walishtuka sana kuona Mbunge ameletwa kwa kesi ambayo haileweki kwahiyo nilikuwa na kazi kama kiongozi ya kuwatuliza”  

February 26, 2018 Mahakama ya Hakimu mkazi Mbeya iliwatia hatiani Sugu na Emmanuel Masonga Katibu wa CHADEMA nyanda za juu kusini na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli, lakini wawili hao waliachiwa huru Mei 10, 2018 kwa msamaha wa Rais Magufuli alioutangaza katika sherehe za sikukuu ya Muungano April 26, 2018.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa