Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Picha zilizotikisa dunia

Jumanne , 13th Mar , 2018

Tuliwahi kukuletea makala ya picha mbali mbali zilizopigwa na waandishi wa habari, ambazo zilitikisa dunia na kuifanya iamke kuliangalia kwa macho tukio hilo, na pengine kutafutiwa suluhu yake.

Leo tunaendelea na picha za matukio mengine, ambayo kwa namna moja au nyingine zimegusa maisha ya watuy na kuacha gumzo kwa jamii.

Mmoja wa waokoaji nchini Syria Abu Kifah akiwa na wenzake, walifanikiwa kumuokoa mtoto mwenye siku 30 tu tangu azaliwe, kwenye vifusi vilivyoanguka kutokana na mashambulizi yaliyokuwa yakiendelea ya vita, katika mji wa Idlib. Baada ya kumuokoa alimkumbatia kifuani kwake kwa hisia huku akitokwa na machozi akiwa anmkimbiza gari la wagonjwa ili apelekwe hospitali, tukio ambalo lilifanikiwa kupatwa vizuri na vyombo vya habari, na kusababisha gumzo dunia nzima juu ya matukio yanayoendelea Syria.

Muokoaji Abu Kifah akitoa machozi baada ya kumuokoa moto mwenye umri wa siku 30 kutoka kwenye kifusi baada ya shambulizi la bomu nchini Syria.

Mnamo mwezi April 2017, ndege ya kivita iliangusha bomu la kemikali kwenye mji wa Idlibi, na kusababisha madhara kwa wakzi wa eneo hilo hukutakriban watu 100 wakiwemo watoto kufariki kwa sumu kali iyotokana na bomu hilo. Mpaka sasa hajajulikana nani anahusika na bomu hilo kati ya serikali ya Syria, Waasi au Russia ambao ni supportes wakubwa wa serikali ya Rais wa Syria Bashar al-Assad.

 

Watoto waliouwa kwa bomu la sumu nchini Syria

Karibia Afrika nzima na dunia tunafahamu kilichotokea nchini Rwanda mwaka 1994, juu ya mauaji ya Kimbari, Wahutu na Watutsi walivyokuwa wanauana. Tukio ambalo mpaka leo limeacha alama kwenye maisha ya Wanyarwanda wengi hata nchi jirani za Afrika Mashariki. Picha hii inaonyesha miili ya watu waliokufa ikiwa imelala nje ya kanisa huko Lukara, ikipigwa na mpiga picha Scott Peterson

Masalia ya miili ya watu wa Rwanda ikiwa imelala mbele ya kanisa

Mwaka 2017 haukuwa mzuri kwa jirani zetu Kenya kufuatia machafuko kadhaa yaliyojitokeza, kutokana na uchaguzi wa Agosti 8. Picha hii ilipigwa na Brian Ganga ikimuonyesha askari polisi akitokwa na machozi, baada ya kushuhudia askari mwenzake akimpiga risasi raia, wakiwa kwenye vurugu. Picha hii ilisambaa sana kwenye vyombop vya habari Afrika na kuacha gumzo kubwa.

Askari akilia kwa kutoa machozi baada ya kushuhudia tukio la mtu kuuawa

Mwaka 2012 tasnia ya habari Tanzania ilipigwa pigo kubwa sana baada ya mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi wa mkoani Iringa, kuuawa kikatili na polisi. Picha hii ilipigwa na Joseph Senga (marehemu pia) ikionyesha tukio zima jinsi Daudi Mwangosi alivyouawa kwakupigwa bomu na Polisi. Wahusika walikamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kufikishwa mahakamani na kuhukumiwa miaka 15 jela.

Polisi wakiwa wamemzunguka mwandishi Daudi Mwangosi kabla hajauawa

 

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali