Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi Pwani yaua majambazi wanne

Ijumaa , 12th Jul , 2019

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani, limefanikiwa kuua majambazi wanne katika tukio la majibizano ya risasi, baina ya polisi na majambazi hayo huko eneo la Kwala, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa polisi mkoani humo, Wankyo Nyigesa, ambapo amesema, tukio hilo limetokea Julai 11,2019, majira ya saa 8 mchana baada ya kupata taarifa ya uwepo wa watu, waliopanga kwenda kuvamia na kupora fedha za malipo, kwa wafanyakazi wanaojenga Bandari Kavu ya Kwala.

"Jeshi la Polisi Mkoani hapa tuliweka mtego, na majambazi hao kujikuta wakinasa, na kuanzisha majibizano ya risasi na kupelekea majambazi wanne, kati ya sita wanaodhaniwa kuwepo kupoteza maisha" amesema RPC Wankyo.

Katika tukio hilo, majambazi hao wamekutwa wakiwa na bunduki mbili aina ya Pump action, Radio call moja, hirizi, dawa za kupulizia watu, kamba za kufungia watu na, Plasta za kuziba watu midomoni.

Vitu vingine ni pamoja na leseni za udereva, vitambulisho mbalimbali vya uraia, kadi ya bima ya afya, koti, kaniki, kanzu, suruali na kaptula .

Miili ya majambazi hao, imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Tumbi.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa