Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi wadai Mbowe alilewa, wamtaja Joyce Mukya

Ijumaa , 12th Jun , 2020

Jeshi la Polisi nchini limesema upelelezi wa tukio la kushambuliwa kwa M/kiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, limebaini kuwa eneo la tukio kulikuwa na watu ambao wangeweza kusikia lakini hawakuona tukio lolote na hata alipofikishwa Hospitali alikuwa kalewa chakari na kushindwa kutamka maneno.

Kulia ni Msemaji wa Jeshi la Polisi, SACP David Misime na kulia ni M/Kiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe.

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi hilo SACP David Misime, na kuongeza kuwa  kwa mujibu wa maelezo ya Mbowe alisema kuwa tukio hilo lilimpata majira ya saa 7 usiku, wakati akitokea kwa mzazi mwenzake Joyce Mukya, na hata baada ya tukio kutokea walimpigia yeye na hakuona umuhimu wa kupiga simu Polisi.

"Uchunguzi wetu umethibitisha kuwa siku ya Juni 8, 2020, Mbowe alitembelea sehemu kadhaa za starehe zinazouza vileo ikiwemo Royal Village, na kupata kilevi na hata alipofika hospitalini alionekana akiwa kwenye hali ya ulevi chakari, kiasi cha kushindwa kutamka maneno sawa sawa" amesema SACP Misime.

Aidha ameongeza kuwa "Upelelezi wetu umepata ushahidi wa kutosha kutoka kwenye eneo la tukio unaoonesha kuwa kulikuwa na watu ambao kwa namna yoyote, wangeweza kusikia makelele yaliyopigwa na Mbowe kuomba msaada, lakini kwa mujibu wa mashahidi hakuna hata mmoja aliyeweza kusikia kelele wala kuona tukio la Mbowe kushambuliwa".

Tazama video hapa chini.

 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa