Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Prof. Mbarawa aingilia kati mgogoro wa KIA

Jumamosi , 24th Sep , 2016

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka wananchi wanaozunguka eneo la uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho Serikali inatafuta ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka wananchi wanaozunguka eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho Serikali inatafuta ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro kati yao na mwendeshaji wa uwanja huo kampuni ya KADCO.

Prof Mbarawa mgogoro huo uliopo kati yao na mwendeshaji wa uwanja huo kampuni ya KADCO, ufumbuzi utakaopatikana utakuwa na manufaa kwa pande zote na kujali maslahi ya Taifa.

"Msiwe na wasiwasi Serikali yenu ni sikivu, tutayakagua maeneo yote na kuangalia maslahi ya pande zote na kutoa maamuzi yenye manufaa kwa wote", amesisitiza Prof. Mbarawa.

Mgogoro kati ya wananchi wanaozunguka uwanja wa ndege wa KIA na kampuni ya KADCO ambao umekuwako toka mwaka 1998 umesababisha misuguano na hisia kali kwa muda mrefu hali iliyosababisha Serikali kuamua kuupatia ufumbuzi wa kudumu.

Waziri Prof. Mbarawa ametuma timu ya wataalamu kupitia eneo lote la uwanja wa ndege huo lenye kilomita za mraba 110 katika siku mbili kuanzia sasa ili kuangalia wadau wote walioko ndani ya eneo hilo, athari zake kwa uwanja na wananchi kabla ya kutoa uamuzi wa mwisho.

Katika hatua nyingine Prof. Mbarawa ameitaka KADCO kuongeza mapato katika uwanja wa ndege wa KIA ambao ni wa pili kwa ukubwa hapa nchini ili kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuongeza mapato katika sekta zote za kiuchumi.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton