
Pichani mtu akiwa amefungwa pingu (Picha kutoka mtandaoni)
Hukumu hiyo imetolewa hii leo na Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustina Mmbando na kusomewa mashtaka na wakili wa serikali Sitta Shija.
"Faini milioni mbili kwa kila kosa au kwenda jela miezi sita kwa kila kosa" amesema Mmbando
Katika kesi hiyo mshtakiwa anadaiwa kuingia na kukutwa akiishi nchini bila kibali ambapo alikiri kutenda kosa hilo.
Aidha mshtakiwa ameshindwa kulipa faini hiyo na amerejeshwa rumande.