
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima,akiwa na mtoto Victor
Akitoa Salamu za Rais Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, wakati wa kumkabidhi bendera ya Taifa mtoto Victor Paschal Tantau, anayetarajiwa kushiriki Mkutano wa Jukwaa la Watoto Duniani utakaofanyika nchini Denmark kuanzia tarehe 13 hadi 16 Septemba, 2022.
Amesema kuwa Watoto wanastahili haki ya kushiriki na kushirikishwa kwenye masuala yanayowahusu. ikiwa ni kutekeleza Haki hiyo ya Msingi kwao na inayotambuliwa na Baraza la Usalama la Umoja la Umoja wa Mataifa likihusisha viongozi wa nchi wanachama wa Umoja huo kwenye mkutano maalum iliofanyika tarehe 8 hadi 10 Mei, 2002 ikiwa na maazimio kadhaa likiwemo azimio la kuunda chombo maalum kwa ajili ya ushiriki na ushirikishwaji wa Watoto katika masuala yanayowahusu.