Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ratiba kuagwa wanafunzi wa UDSM kesho

Jumatano , 13th Jun , 2018

Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), imetoa taarifa ya kukatisha ratiba ya masomo kwa muda wa masaa matatu kesho Juni 14, 2018 ili kutenga muda wa kuaga miili ya waliokuwa wanafunzi na watumishi wa chuo hicho.

Taarifa hiyo imetolewa leo Juni 13, 2018 na Ofisi ya Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma Profesa Bonaventure Rutinwa na kuongeza kuwa masomo yatasitishwa kuanzia Saa 4:00 asubuhi mpaka 7:00 Mchana.

Taratibu za kuaga miili ya marehemu zitafanyika katika ukumbi wa Nkrumah uliopo chuoni hapo siku ya kesho Juni 14, 2018 kuanzia Saa 4:00 Asubuhi.

Katika ratiba ya kutoa heshima za mwisho kwa marehemu hao inaonesha, waombolezaji wataanza kuingia katika ukumbi wa Nkrumah kuanzia saa 3:00 asubuhi, na ikifika 3:45 miili ya marehemu hao itaingia ukumbini, ambapo shughuli ya kuaga itaanza rasmi saa 5:40 asubuhi mpaka 6:50 Mchana.

Juni 11, 2018 katika eneo la Riverside-Ubungo wanafunzi wawili na watumishi wawili wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), walifariki Dunia baada ya gari la wagonjwa walilokuwa wamepanda kugoganga na lori la mizigo walipokuwa wanaenda katika Hospitali ya Chuo hicho kwa matibabu.

Waliofariki kutokana na ajali hiyo ni wanafunzi Erasto Sango Steven na Mary Godian Soko na watumishi wawili James Rutayuge ambaye alikuwa ni dereva pamoja na muuguzi msaidizi daraja la pili Jonathan Lung’ando.

 

 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa