Ijumaa , 6th Mei , 2022

Kamati ya ulinzi na Usalama iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe imekamata magari 14 yanayosafirisha magenzo likiwemo gari moja linamilikiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Mkuu wa mkoa wa Songwe Omary Mgumba amesema kuwa kuwa gari hilo lilikuwa ofisini ndipo dereva wa gari hilo alipodanganya ofisini kuwa ana dharura na akaruhusiwa kutoka na gari ndipo akaenda kufanyia shughuli hizo

Aidha mkuu huyo wa mkoa wa Songwe amesema kuwa wataendelea kuwashikilia na kuwakamata wamiliki wote wa magari hayo na hawatayatoa hadi pale watakapowaleta madereva wote waliokua wanaendesha magari hayo

Aidha Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Songwe ametoa wito kwa Wafanyabiashara, kufuata sheria za forodha ili kuepuka kukamatwa na magendo na sheria kuchukua mkondo wake