Jumanne , 1st Dec , 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge ametangaza kufanya mkutano wa wawekezaji na wafanyabishara wa  mkoa wa Dar es salaam ili kubaini changamoto mbalimbali na namna ya kuzitatua.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam amesema bado mkoa huo unafursa ya kuongeza pato licha ya kutokuwepo kwa rasilimali Kama madini na vinginevyo Kama mikoa mingine.

''Bado mkoa una fursa ya kuongeza pato, Mkoa na Serikali tarehe 10 tutakua na mkutano na wenye viwanda na wafanyabishara  lengo ni kutoa mrejesho wa  Serikali imefanya nini maeneo yenye changamoto na ambayo bado, yako kwenye hatua gani''amesema RC Kunenge

Aidha ameongeza kuwa wanaamini kwa kufanya hivo kutaongeza ajira kwa wananchi na kudai kuwa huduma zinazozalishwa zitasaidia kutatua mahitaji mbalimbali katika jamii.