Jumanne , 24th Mei , 2022

Jeshi la Rwanda limesema kuwa wananchi kadhaa wa Rwanda wamejeruhuiwa kufuatia mabomu yaliyorushwa mpakani na majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Jeshi hilo limesema kuwa linafanya uchunguzi kwenye eneo hilo kuhusu shambulizi hilo. .

Mgongano baina ya nchi hizo mbili umeongezeka toka mwezi March, wakati vikosi vya  waasi wa  M23 ambavyo Congo inaishutumu Rwanda kwa kuviunga mkono, vilipowashambulia wanajeshi wawili wa Congo.  
Hata hivyo Rwanda imekua ikikana madai kwamba inawasaidia waasi hao.

Kundi hilo la waasi limekua  likiisumbua  serikali ya  Congo  toka mwaka 2012 na mwaka 2013.  
Familia nyingi zimekimbia makazi yao huko kaskazini mwa jimbo la Kivu, zikielekea kwenye mpaka wa Uganda  majini Bunagana.

Mkuu wa shirika la umoja wa mataifa linaloshugulikia wakimbizi nchini Uganda, Joel Boutroue, amesema kuwa  maelfu ya wakimbizi wamewaili nchin iUganda siku ya jana