Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sababu za kukithiri kwa matukio ya watu kujiua

Jumanne , 18th Sep , 2018

Zama zinabadilika na maisha yanabadilika pia, limekuwa ni suala la kawaida hivi sasa kusikia mtu amemuua rafiki yake, ndugu yake, mke au familia yake yote tena kikatili kabisa .

Kwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO), utafiti unaonesha watu takribani 1000,000 hupoteza maisha kila mwaka kwa kujiua, ambao ni sawa na watu 3000 kwa kila mwezi na mtu mmoja kila baada ya dakika 40. Vijana wenye umri miaka 15-25 ndiyo wanaoongoza kwa matukio hayo.

Hali hiyo iko pia katika nchi ya Tanzania, ambapo katika kipindi cha Funguka kunachoruka kupitia EATV na ukurasa wa Facebook, wadau mbalimbali wametoa sababu mbalimbali zinazochangia kukithiri kwa matukio hayo katika maeneo yao  kwenye mada iliyouliza “NINI SABABU INAYOPELEKEA KUKITHIRI KWA MATUKIO YA WATU KUJIUA NA KUUA FAMILIA ZAO” na haya ndiyo maoni yao.

Robius wa Mjungu: Wa Kagera, Karagwe tz. Zipo sababu nying zifuatzo ni baadhi, 1 ni kuwa na msongo wa mawazo, 2 ni kuwa na ugumu wa maisha, 3 ni kutokua na moyo wa subira, mfano mwanamfunz akiwa amefeli.

Kelvin John Nyamuga: Wa Mwanza, mi nafikiri mpaka mtu kufikia hatua hiyo kuna mambo yanamchanganya na pa kuyaweka hakuna au hakuna wa kushirikiana nae kimawazo!.

Katoto Ever:  Wa Kurasini, Polisi ufundi...huwa ni matatizo ya kisaikolojia maana bora ukutane na mtu mwenye tatizo la akili ni raisi kumgundua kwani anaweza kuvaa viatu kichwani ila ambaye hana tatizo la kisaikolojia sio raisi kumtambua kwani huwa yuko smart na hawa ndio wakishafanya tukio Jamii mzima itabaki ikishangaa.

Zainabu Issa Kibirity: Wa Mi naona mtu anachukua maamuz hayo kwa msongo wa mawazo na akifikiria hana wa kumpa msaada wala nini, sasa unafikiri hapo utatamani kuishi.

Camila Mroso: Ugumu wa maisha unachangia kwa kiasi kikubwa.

Hammy de Love: Wa Morogoro, #funguka ni tamaa tu za kifedha na ugomvi wa kijinga ndicho kinachosababisha watu wengi kujiua ama kuuwa wenzao.

Juniour Silver: Mimi naona ni ugumu wa maisha kwa sasa na pia ni kutokana na kutokuwana maelewano ndani ya familia, ugomvi ndani ya nafsi ya mtu na ukosefu wa elimu katika jamii. Toka pande za moshi, mabogini juniour a.k.a yakuza juniour 11.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa