Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sekretarieti ya Halmashauri kuu CCM kukutana leo

Jumanne , 19th Jul , 2016

Maandalizi ya mkutano mkuu maalum wa kumchagua mwenyekiti mpya wa Chama Cha Mapinduzi yamekamilika ambapo wajumbe wa Mkutano mkuu huo wamehakikishiwa usalama wa kutosha katika kipindi chote cha mkutano huo.

Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka.

Hayo yameelezwa na Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa makao makuu ya CCM mjini Dodoma na kusema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuhakikisha usalama kwa wajumbe wote wa mkutano huo.

Amesema mkutano huo utatanguliwa na kikao cha sekretarieti ya Halmashauri kuu ya taifa ambacho kitakutana leo na kufuatiwa na kikao cha kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ambayo itakutana Julai 21 ambapo kikao cha Halmashauri kuu ya Taifa kitakutana Julai 22 na kupendekeza jina la mgombea uenyekiti wa chama hicho na kulipeleka kwenye mkutano mkuu.

Amesema Mkutano mkuu maalum wa kumchagua mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi utafanyika Julai 23 mwaka huu ambapo jina la Rais Dk John Pombe Magufuli limependekezwa kugombea nafasi hiyo ambapo atapigiwa kura ya ndiyo na hapana.

Jumla ya hotel 306 na vyumba 3,331 mjini Dodoma vimeshachukuliwa kwa ajili ya wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa kumchagua mwenyekiti wa chama hicho huku ikitegemewa zaidi ya wajumbe 2,000 kuhudhuria katika mkutano huo pamoja na wageni waalikwa.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa