Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yaagiza kuanza ujenzi madarasa nchi nzima

Jumapili , 24th Jan , 2021

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde ameagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekaa chini kwa kukosa madawati au kusoma chini ya miti kwa upungufu wa madarasa na kuagiza ujenzi wa madarasa-

Picha ikiwaonesha wanafunzi kutoka moja ya shule nchini (picha na mtandao) kulia ni Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde.

katika wilaya zote uanze mara moja kwa yale maeneo yenye upungufu wa madarasa.

Silinde ametoa maagizo hayo alipotembelea shule ya msingi King'ongo iliyopo wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es Salaam kufatia agizo la Rais Dkt. John Magufuli la kutaka ujenzi wa madarasa ya shule hiyo ukamilike kwa haraka, baada ya kuona video ya watoto wa shule hiyo wakisoma chini ya mti.

Silinde amesema serikali ilitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa maeneo mengi ya nchi katika mradi wa lipa kwa matokeo EP4R tangu mwezi wa Juni, 2020 lakini madarasa bado hayaja kamilika katika baadhi ya maeneo lakini kwa ujenzi wa madarasa katika shule ya King'ongo utakamilika ndani ya wiki zisizozidi tatu na kutaka watendaji katika wilaya zote kukamilisha ujenzi bila kusukumwa na viongozi wa kubwa wa nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo  Beatrice Dominic amemwambia Naibu Waziri wa TAMISEMI kuwa ujenzi wa madarasa huo utakamilika Januari 31, 2021 na hadi Februari  5, wanafunzi wataanza kuyatumia madarasa hayo na mpaka kukamilika yatatumia zaidi ya shilingi milion 205 yakiwa ni ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa ambavyo vitakuwa na madawati yake pamoja ujenzi wa choo chenye matundu 12.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa