Ijumaa , 21st Oct , 2022

Mtendaji Mkuu wakala ya maabara ya Veterinari Tanzania TVLA Dk.Stella Bitanyi amewatoa hofu walaji wa kitoweo cha Nguruwe (Kitimoto) ambacho kwa siku za hivi karibuni iliibuka hofu kwa walaji kuhisi nyama ya mnyama huyo kuwa na wadudu wenye madhara kwa afya ya binadamu

Dk.Stella Bitanyi amesema mnyama huyo nikama wanyama wengine hivyo akitunzwa na kuandaliwa vizuri hana madhara lakini kama hatatunzwa vizuri nikweli ana wadudu wenye madhara

Katika hatua nyingine Dk.Bitanyi amesema inakadiriwa kwamba kufikia mwaka 2030, watu zaidi ya milioni 10 watakufa kila mwaka kutokana na dawa kushindwa kuwatibu kwani vimelea vya magonjwa vitakuwa vimejenga usugu unaotokana na matumizi holela ya dawa kwa binadamu na mifugo