Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yazungumzia ripoti ya uchunguzi wa Lissu

Ijumaa , 14th Sep , 2018

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndio wanachelewesha kukamilika kwa ripoti ya uchunguzi dhidi ya shambulio la mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Waziri Masauni ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali laMbunge wa Ubungo (CHADEMA) Saed Kubenea bungeni leo Septemba 14, ambalo lilihoji kuwa kumekuwa na matukio mengi ya kihalifu yanatokea ikiwemo kupotea na kutekwa watu, lakini serikali imekuwa ikionesha kuwalinda zaidi watu wao wa karibu na sio wanaharakati wanaoipinga serikali na kuhoji ni lini ripoti ya serikali itakamilika kuhusiana na tukio la kushambuliwa kwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Masauni amemtaka Kubenea kufuta kauli yake aliyodai kuwa ni upotoshaji kwa jamii kwani hakuna matabaka katika ulinzi wa raia na mali zao na kusema kuwa “Napenda kujibu swali la Kubenea lakini ningependa kumpinga na kumkosoa vikali kwa kauli yake, kwani hakuna matabaka katika kulinda na kusimamia usalama wa raia na mali zao wote na hakuna matabaka, kuhusu shambulio la Tundu Lissu chama chao hakitoi ushirikiano ikiwemo kumficha dereva ambaye ndiye shuhuda namba moja”.

Aidha Masauni ameongeza kuwa masuala ya kigaidi yanahitaji muda zaidi kukamilisha uchunguzi wake kwakuwa huhusisha taasisi nyingine za nje zaidi ya Jeshi la polisi hivyo unahitaji muda na umakini wa hali ya juu.

Suala la watu wasiojulikana limekuwa likiibua mvutano bungeni kila ifikapo zamu ya kuchangia kwa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kuibuka kwa matukio ya utekaji na kupotea kwa watu maarufu kuanzia mwaka 2017 wakiwemo wanahabari na wasanii wa muziki.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali