Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yatoa onyo kali

Jumatatu , 13th Nov , 2017

Serikali imelionya baraza la madiwani la Manispaa ya Kigoma Ujiji kuacha mara moja kushiriki kwenye Mpango wa Kimataifa wa uendeshaji wa shughuli za serikali kwa uwazi (OGP), ambao serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejitoa.

Onyo hilo limetolewa leo bungeni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Mh. Goerge Mkuchika wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe lilitoka kujua kauli ya serikali kutokana na ushiriki wa Manispaa hiyo kwenye mpango huo.

“Serikali inazo taarifa kuwa Manispaa ya Kigoma Ujiji mpaka sasa inawasiliana na OGP na OGP wamemwandikia barua Waziri wa mambo ya Nje  kwamba wana nia ya kuendelea kushirkiana na nyie, sasa nataka niionye Manispaa ya Kigoma Ujiji waache mara moja kuwasiliana na OGP”.

Aidha Waziri ameitaka Manispaa hiyo kutekeleza maamuzi ya serikali na endapo itaendelea basi serikali itachukua hatua kali ambazo ni kuvunja baraza la madiwani na kuweka Tume ya Manispaa. 

Waziri pia ameeleza kuwa taratibu za OGP zipo wazi kuwa nchi ikijitoa moja kwa moja ushiriki wa wanachama wengine kutoka ndani ya nchi husika unakuwa umefika kikomo hivyo Manispaa hiyo inavunja kanuni za nchi.

Tanzania imejitoa kwenye Mpango wa Kimataifa wa uendeshaji wa shughuli za serikali kwa uwazi (OGP), ambao imedumu kama mwanacham kwa miaka minne tangu ilipojiunga Septemba 21 mwaka 2011.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa