Bodi ya Mikopo
Kauli hiyo imetolewa leo Juni 22, 2021, Bungeni Dodoma na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, na kuongeza kuwa kiwango hicho cha pesa kitawanufaisha wale wanafunzi 11,000 walioshindwa kuendelea na masomo kwa mwaka jana na wale wa mwaka huu wanaokadiriwa kuwa 10,000 kutokana na kukosa mkopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini (HESLB).
"Mwaka jana takribani wanafunzi 11,000 wale wenye sifa waliokosa masomo kwa sababu ya mkopo na wazazi wao hawana uwezo na wakabaki majumbani na mwaka huu 10,000, wanakadiriwa wangekosa mkopo, tunapendekeza kuongeza shilingi bilioni 70 kwenye zile bilioni 300 ambazo zitawapeleka wote," amesema Dkt. Waziri Nchemba.