
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Ali Mohammed Shein
Dk. Shein ametoa changamoto hiyo mjini Zanzibar wakati akiwahutubia wafanyakazi wa serikali zote mbili katika hotuba yake ya siku ya wafanyakazi duniani hapo jana.
Mapema wakitoa risala yao ya shirikisho la wafanyakazi wametaka haja ya kuheshimiwa mikataba ya kimataifa na haki zao, kutambuliwa na serikali, huku mwenyekiti wa shirikisho hilo Bw. Zaharani Mohamed Nassor akiitaka serikali kupunguza kodi kwa vile zimekuwa nyingi na zinawatesa wafanyakazi.