Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Shule zilizojipanga kufanya udanganyifu zatajwa

Jumatatu , 23rd Nov , 2020

Jumla ya wanafunzi wa kidato cha nne 490,103, wamesajiliwa kufanya mitihani ya kumaliza elimu yao ya sekondari, ambayo imeanza kufanyika hii leo na kati yao watahiniwa wa shule 448,164, na watahiniwa wa kujitegemea ni 41,939.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde.

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde, na kusema kuwa kati ya watahiniwa wa shule 448,164, waliosajiliwa, wavulana ni 213, 553 sawa na asilimia 47.7, na wasichana ni 234,611, sawa na asilimia 52.3, huku wenye mahitaji maalum ni 893 na kati yao, 425 ni wenye uoni hafifu, 60 ni wasioona, 186 wenye ulemavu wa kusikia na 222 ni wenye ulemavu wa viungo vya mwili.

Aidha Dkt. Msonde, alivitaja vituo ambavyo vimeripotiwa kujipanga kufanya udanganyifu, katika mitihani inayoanza hii leo katika mikoa mbalimbali hapa nchini, ikiwemo shule ya sekondari Itundu, Mpesu, Wenda, Swila, Onicah, Ntonzo, St Marcus na Kipoke zote za mkoani Mbeya.

Shule zingine ni Geita Adventist na Waja Boys za mkoani Geita, Mary Goret, Agape Junior Seminary, Ebenezer Sango, GreenBird, Mema, Oshara, Sanya Juu na Seuta zote za mkoani Kilimanjaro, Fidel Castrol, Shamiani, Madungu zote za kusini Pemba, pamoja na Mwembeni, Morembe, Marshi na Paroma zote za mkoani Mara.

Shule zingine ni za mkoani Ruvuma, Morogoro, Mjini Magharibi, Mwanza, Simiyu, Mtwara na Songwe. 
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi